Wajibu wa daktari ni kutibu; uponyaji anatoa Mungu;
Wajibu wa mwalimu ni kufundisha; uelewa anatoa Mungu;
Wajibu wa Mchungaji ni kuhubiri; wokovu anatoa Mungu;
Wajibu wa kulala ni wako; usingizi anatoa Mungu;
Wajibu wetu ni bidii kazini; mafanikio anatoa Mungu;
Wajibu wa dereva ni kuendesha; kufika ni majaaliwa ya Mungu;
Wajibu wetu ni kuoana; kupata watoto ni wa Mungu;
Wajibu wetu ni kuomba; majibu ni kazi yake Mungu;
Kabla ya kuomba lazima ujitathmini kwanza kama umetimiza wajibu wako.
Kumuomba Mungu akuponye na wakati hujafika kwa daktari ni utani;
Kumuomba Mungu akupe utajiri na wakati unalala muda wote ni utani;
Kuomba ufaulu mtihani na wakati husomi ni utani;
Kuomba amani ya ndoa na wakati huna adabu kwa mpenzi wako ni utani;
Siyo kwamba Mungu hawezi kufanya bila wewe kufanya. Hapana!
Mungu ni Shirikishi. Anaheshimu uwezo aliokuwekea ndani yako;
Wewe fanya kulingana na urefu wa kamba yako, kisha mtwike yeye;
Mungu alipoumba mto, alituachia kazi ya kujenga daraja
Angeweza sema alitupa heshima ya kushiriki.
Hamasa Jukwaani, nicheki kupitia https://wa.me/message/53VBBZFVGUZWF1
0 Comments